Wednesday, 23 December 2015

JE, NI AFUENI SASA KWA WETANGULA?

NA JULIUS KARIITHI


Seneta wa Bungoma Moses Wetangula,


Mahakama ya juu imesimamisha kituo cha BBC kutomhusisha seneta wa Bungoma Moses Wentagula, na madai ya kuhongwa na kampuni ya sigara ya British American Tobacco  (BAT)
Wetangula  kwa ombi lake la dharura, kwa mahakama ya juu, alisema kuwa kituo hicho kilimharibia jina katika kipindi chao kijulikanacho kama Panorama, ambacho kinadai kuwa seneta huyo  aliomba kukatiwa tikiti ya ndege, kwa niaba ya mkewe kwenda London kwa njia isiyo wazi.
Kulingana na senator huyo, kipindi hicho kilitangaza kuwa yeye alihusishwa na ufisadi, ambapo alishirikiana na kampuni ya BAT na kumhonga wakati alipokuwa akihudumu kama waziri wa biashara ,katika enzi za rais mstaafu Daniel Arap Moi.

Senator huyo kupitia mshauri wake mkuu ,James Orengo,  alisema kuwa taarifa hiyo iliyo peperushwa na BBC, imezidi tutambaa katika mtandao wa kijamii , runinga pamoja na televisheni ,jambo ambalo limesababisha yeye kuchukiwa bure.


No comments: