![]() |
Gavana Nderitu Gachagua. |
Na Mwangi K.Githinji.
Hoja ya kumuondoa mamlakani gavana wa Nyeri Nderitu
Gachagua imepitishwa na wawakilishi wa kaunti hiyo.
Kulingana na spika wa bunge hilo Mwangi Mugo ni kuwa
hakuna aliyepinga mswada huo kwenye bunge hilo huku wote wakiiunga
mkono kwa pamoja.
Amesema kuwa hatua itakayofuata ni kuwasilisha
uamuzi huo kwa bunge la seneti ambalo
sasa litachukua hatamu kwa kutengeneza kamati
itakayofanya uamuzi kuhusu hatma ya Gachagua.
Wawakilishi hao wanamshtumu gavana huyo kwa kutotii
mamlaka ya bunge hilo,Kutumia fedha za kaunti vibaya na kushindwa kwake kupitisha
bajeti na vile vile matumizi mabaya ya afisi yake.
Mwanzoni wawakilishi wanaomuunga mkono gavana Gachagua
waliondoka katika kikao cha leo baada ya mawakili wake kunyimwa nafasi ya kuhudhuria
kikao hicho.
No comments:
Post a Comment