Usalama unazidi kuimarishwa katika uwanja wa kimataifa wa
ndege wa jomo Kenyatta, kufwatia ziara ya rais wa Marekani Barrack Obama.
Maafisa wa usalama wanashika doria katika uwanja huo kwa
lengo la kuimarisha usalama kabla ya kuwasili kwa Raisi Barack Obama mwendo wa
saa mbili unusu leo usiku.
Wanafunzi wa shule ya upili ya Makini wametamatisha
maandalizi yao ya kumtumbwiza rais Obama
katika ikulu ya rais hapo kesho.
Baadhi ya barabara atakazo tumia rais Obama zishafungwa
ikiwemo ile ya Waiyaki,chiromo na barabara kuu ya kuelekea Mombasa huku
barabara kuu ya Thika na ya Limuru zikitarajiwa kufungwa baadae hapo kesho na
jumapili.
Hata hivyo nyanyake rais Obama mama Sarah amewasili hapa
jijini katika ndege ya shirika la Kenya airways,huku akitarajiwa kukutana na
rais Obama pindi tu atakapowasili katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta.
Wananchi kutoka eneo la Kogelo kaunti ya Siaya watakuwa
wakifwatilia matukio ya Rais Obama moja kwa moja kutoka kwenye runinga kubwa zitakazowekwa
katikati mwa mji. Hii ni baada ya
kusemekana kuwa rais Obama hatazuru eneo
hilo.
Tutakupasha matukio yote kulingana na ziara hiyo pindi tu
yatakapojiri,
Kumbuka unapata matangazo hayo katika steshenu yako nambari
moja ya kijamii ECN Radio…
Tuskize kupitia tufuti yetu ya www.mixlr.com/ecn-radio
No comments:
Post a Comment