![]() |
Raila Odinga, Agnes Zani na maafisa wengine wa ODM |
Hii ni
kutokana na kufujwa kwa takriban shilingi milioni hamsini na moja katika kaunti
ya Kilifi, inayoongozwa na gavana Amason Kingi kisha Odinga kumtetea Kingi.
Odinga
akiongea katika makao yake makuu yaliyo Capital Hill hapa jijini Nairobi akiwa
ameandamana na zaidi ya wabunge kumi wa ODM, Raila alisema kuwa hajajaribu
kuwatetea magavana wafisadi katika muungano wa CORD kama ilivyodaiwa na
kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Aden Duale, akikariri kuwa serikali
ya Kilifi ilichukua hatua kwa kuwatimua maafisa fisadi katika kaunti hiyo.
Duale hata
hivyo ametetea madai yake huku akisema kuwa ana ushahidi wa kutosha kumhusisha
Raila na ufisadi katika kaunti anazoongoza ingawa mwakilishi wa kina mama
katika kaunti ya Mombasa Mishi boko amemtetea Odinga.
No comments:
Post a Comment