Wednesday, 17 August 2016

SAJILI MPYA MANE APELEKWA HOSPITALINI.


Mchezaji wa Liverpool Mane.
Na Mwangi K. Githinji.

Sajili mpya wa Liverpool Sadio Mane alipelekwa hospitalini Kusini mwa Liverpool ili kufanyiwauchunguzi kwenye bega lake baada ya kupata jeraha akiwa mazoezini.
Inaripotiwa kuwa mchezaji huyo aliondoka Liverpool akiwa amefungwa mkononi mwake ishara kuwa alikuwa ameumia japo inakisiwa kwamba jeraha hilo sio mbaya sana.
Katika mechi yao ya mwisho sajili huyo mpya alionyesha viwango vizuri vya mchezo katika ushindi wao wa mabao 4-3 dhidi ya arsenal ambapo pia alifunga goli.
Liverpool wanajiandaa kuchuana na Burnely katika mechi yao ijayo ya ligi.


No comments: