Monday, 29 August 2016

STEPHEN SOI KUFIKISHWA MAHAKAMANI LEO

Stephen Soi aliyekuwa mkuu wa Kikosi cha Kenya kilichoshiriki Olimpiki Rio
Ben Kirui

Aliyekuwa mkuu wa kikosi cha Kenya kilichoshiriki mashindano ya Olimpiki jijini Rio nchini Brazil Stephen Soi pamoja na maafisa wengine wawili wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo kujibu mashtaka mbalimbali kuhusiana na jinsi wanariadha wa Kenya walivyodhalilishwa kule Rio.

Soi ambaye aliachiliwa huru kwa dhamana ya elfu hamsini, naibu wake James Chacha pamoja na katibu mkuu wa kamati ya kitaifa ya Olimpiki Nock Paul Francis walikamatwa ijumaa punde tu walipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa JKIA kutoka Rio na kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga.


Haya yanajiri huku shinikizo za kutaka waziri wa michezo Hassan Wario kujiuzulu zikiendelea kutokana na usimamizi mbaya wa wanaridha wa Kenya.

No comments: