Thursday, 7 April 2016

RAILA AKWEPA WAANDISHI WA HABARI BAADA YA KUWASILI NCHINI

Kinara wa Cord Raila Odinga akikaribishwa na Rais wa Tanzania John Magufuli

Ben Kirui

Kinara wa Cord Raila Odinga amerejea nchini kutoka Tanzania huku mjadala kuhusu sababu yake ya kususia kuhudhuria hafla ya uzinduzi wa azma ya Seneta wa Bungoma Moses Wetangula kugombea kiti cha urais ukishika kasi.
Raila amekwepa waandishi wa habari punde tu alipowasili nchini kutoka ziara yake ya siku tatu kwa Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli.
Kulingana na wandani wake wa karibu, Raila alibadilisha mipango yake siku ya jumamosi alipokuwa akielekea Kakamega kwa sababu ya ripoti za kuzuka kwa ghasia katika bustani ya Muliro Gardens ambapo mkutano wa Wetangula ulikuwa ukifanyika.


No comments: