Monday, 7 November 2016

MWANAFUNZI AFARIKI MUDA MFUPI KABLA YA KSCE

Mtihani wa mwaka huu unafanywa chini ya uangalifu mkali kuzuia udanganyifu kama ulivyoshuhudiwa mwaka jana
Racheal Kithaka
Mwanafunzi wa kidato cha nne amefariki huko Nakuru muda mfupi kabla ya kuanza kwa mtihani wa KCSE mapema leo. 

Mkurugenzi wa elimu kaunti ya Nakuru Ester Muiru amedhibitisha kifo cha mwanafunzi huyo Francis Gikonyo wa shule ya upili ya Jomo Kenyatta eneo la Bahati. 

Muiru anasema mwanafunzi huyo aliugua muda mrefu na akafariki akipokea matibabu hospitalini.

No comments: