Monday, 7 November 2016

JE, NGILU ATAJIUNGA NA MUUNGANO WA CORD?

Ngilu asemezana na Kalonzo
Robert Mwangi

Kiongozi wa chama cha NARC Charity Ngilu amesema kuwa serikali ya Jubilee imeshindwa kutimiza ahadi zake huku uchaguzi mkuu ukuzidi kubisha hodi.

Ngilu amesema kuwa mkataba wiliotia kati ya chama chake cha NARC na muungano wa Jubilee uliojumuisha TNA na URP umekiukwa.

Ngilu aidha amesema kuwa mkataba huo uliojumuisha hoja tano zikiwemo haki ya maji kwa kila mkenya, afya na kuinua nafasi ya kina mama, umekosa kutiliwa maanani na viongozi wa Jubilee.

Suala la iwapo Ngilu atajiunga na muungano wa CORD limesalia kitendawili licha ya yake kigogo huyo wa chama cha NARC kuonyesha ishara ya kutaka kufanya kazi na vinara wa muungano wa CORD.


No comments: