Monday, 7 November 2016

MCHEZAJI AINGIA MAFICHONI BAADA YA KUMUUA REFARII

Mwili wa refarii aliyepigwa kichwani na mchezaji mmoja nchini Mexico

KAPEDO JNR

Polisi nchini Mexico wanamsaka mchezaji mmoja wa kandanda anayetuhumiwa kwa kumpiga kichwani refarii wa mechi iliyogaragazwa uwanjani Amigos del Balon mnamo tarehe 6 Novemba 2016, baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu.

Mashabiki waliokua uwanjani walidhani muamuzi wa katikati mwa uwanja alikua amepoteza fahamu, baada ya kugongwa kichwani kwenye tendo hilo la unyama
Juhudi za Wafanyikazi wa Shirika la msalaba mwekundu kujaribu kumuokoa muamuzi huyo hazikufua dafu, baada ya kugundua alikuwa amepoteza uhai wake.

Mchezaji huyo aliingia mafichoni baada ya tukio hilo kwa kutumia gari aina ya Pick-up, wakati refarii alikua akipata matibabu.

Refarii huyo kwa jina Victor Trejo kutoka nchini Mexico alipigwa na mchezaji huyo ambaye alikuwa amepandwa na hasira baada ya kulishwa kadi nyekundu

Tukio hilo lilitokea jumaapili ya tarehe sita mwezi Novemba mwaka elfu mbili kumi na sita, katika uwanja mmoja kwa jina la kihispaniola “Amigos del Balon” utafsiri wake ukiwa “marafiki wa mpira” ambao unapatikana kule Tulancingo nchini Mexico.

No comments: