Tuesday, 8 November 2016

CRISTIANO RONALDO KUSALIA UGANI BERNABEU MIAKA 10 ZAIDI


cr7-na-mtoi
KAPEDO JNR

Cristiano Ronaldo amesema kuwa ataendelea kuchezea miamba wa Uhispania Real Madrid kwa muda wa miaka kumi baada ya kuongeza kandarasi yake uwanjani Santiago Bernabeu

Kandarasi ya mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 31, ilitarajiwa kukamilika mwezi Juni 2018, lakini ameiongeza kwa miaka kumi zaidi hadi Juni 2021.
Mshambulizi huyo ambaye zamani alikuwa akichezea Manchester United, amesema kuwa nia yake ni kukamilisha miaka yake ya kucheza kwenye Ulingo wa Soka
Kwa upande wake rais wa klabu hio Florentino Perez, amesema kwamba anampigia upato Mreno huyo kusalia uwanjaniBernabeu kwa miaka mingi ijayo.
Ronaldo amefungia Real Madrid mabao 371 tangu ajiunge na klabu hio kutoka Manchester United mwaka 2009 na amesaidia klabu hio kutwaa taji la klabu bingwa barani ulaya mara mbili na pia kuiwezesha Madrid kushinda taji la ligi kuu ya Uhispania La Liga.


No comments: