KAPEDO JNR
Watu tisa wameuawa na wengine kumi na moja kujeruhiwa katika mji
mkuu wa Sudan kusini, baada ya kushambuliwa na mtu asiyejulikana
Polisi mjini Juba wamedhibitisha kisa hicho wakisema kuwa mtu
huyo ambaye alikua amefunika uso wake aliwafyatulia risasi watu ambao walikua
wanatazama mechi ya Soka katika runinga wikendi iliyopita
Lengo la shambulizi hilo ambalo lilitokea usiku wa jumaamosi kule
kusini magharibi mwa mji wa Gure hailikueleweka
Taifa la Sudan Kusini limekumbwa na visa vya mashambulizi tangu vita
vikuu vilivyozuka mwezi Disemba 2013
Msemaji wa polisi Sudan Kusini Daniel Justin, amesema kuwa
Uchunguzi unaendelea huku akidhibitisha kuwa watu sita waliuawa katika kisa
hicho na wengine watatu wakaaga walipokua wakikimbizwa hospitalini kwa matibabu,
vita vimekua vikizuka mjini Juba tangu Julai mwaka huu.

No comments:
Post a Comment