![]() |
| Picha: Pierre Emerick Abumeyang' |
KAPEDO JNR
Pierre
Emerick Abumeyang ameibuka kuwa mchezaji bora wiki hii, baada ya kutia kimyani
mabao manne dhidi ya Humburg mnamo tarehe 5 Novemba 2016, katika mechi ya
kuwania taji la ligi kuu ya Ujerumani kwenye uwanja wao wa nyumbani, mechi
ambayo Dortmund ilishinda 5- 2
Abumeyang’ ambaye alizaliwa tarehe 10 Juni 1989, kule LAVAL nchini Ufaransa, ni mshambulizi ambaye huchezea timu ya taifa ya Gabon, na pia huchezea klabu ya Borussia Dortmund ambayo inashiriki katika ligi kuu ya Ujerumani, Bundesliga
Abumeyang’ anajulikana kwa mwendo wake wa kasi na
ubunifu uwanjani, huku akiandikisha rekodi ya kukimbia mita 30 kwa muda wa sekunde
3.7, jambo linalomfanya kuwanyanyasa na kuwaacha hoi mabeki wa klabu pinzani.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka ishirini na saba,
alianza taaluma yake katika klabu ya AC Millan kule nchini Italia.
Kwenye msimu wa elfu mbili na nane Ac Millan
ilimwachilia kwa mkopo kwenda klabu ya Dijon kule nchini Ufaransa, ambako alifungia
timu hio mabao 10
Mnamo tarehe 24 Juni 2009, klabu ya Lille ilitangaza kumsajili mshambulizi
huyo kwa mkopo, lakini baada ya fomu yake kudorora walimtuma kwenda kwa
mahasimu wao FC Monaco.
Kwenye msimu wa 2012- 13, Abumeyang’ alimaliza wa
pili katika mashindano ya kuwania mchezaji bora msimu huo, baada ya kufunga
mabao 19 chini ya Zlatan Ibrahimovic
Ni katika msimu huo ambapo Abumeyang’ alishinda taji
la Mchezaji Bora Barani Afrika
Mnamo tarehe 4 Julai 2013, Abumeyan’ alijiunga na miamba
wa Ujerumani Borussia Dortmund kwa mkataba wa miaka 5
Aidha, Abumeyang’ alicheza mechi yake ya kwanza akiwa
na klabu ya Dortmund dhidi ya mahasimu wao Bayern Munich, kwenye mechi ya
kuwania Kombe la DFL Super Cup, mechi ambayo Dortmund ilishinda kwa mabao 4- 2
Mnamo tarehe 31 Julai 2015, Abumeyang’ aliongeza
mkataba kwenye klabu hio hadi mwaka wa 2022

No comments:
Post a Comment