Tuesday, 22 December 2015

AZIKWA AKIWA AMEKETI, BUNGOMA.

NA JULIUS KARIITHI

Mfano wa sanduku la kuzika marehemu akiwa angali
ameketi, kama ilivyotumika katika mazishi ya Bungoma.
 

Wenyeji wa kijiji cha Mungore kaunti ya Bungoma  walimiminika kwa makumi kushuhudia maziko ya ajabu, ya jamaa mmoja ambaye kulingana na amri ya koti alizikwa akiwa ameketi chini.
Mwenda zake Chrisantus Rapong’o aliyekuwa na umri wa miaka 75, alifuata njia ya marahaba mnamo Septemba na bila kupusa wazee wa kanisa alilokuwa akishiriki wakaaza matayarisho kabambe ya kumpumzisha.
Hata hivyo shughuli yenyewe ilionekana kutatizwa na itikadi za tamaduni yake, wakati jamaa yake ilisisitiza kuwa kulingana na tamaduni ya Abakhibe, wanaume wanastahili kuzikwa wakiwa wangali wameketi.
Mzozo huo ulizua tofauti nyingi baina ya wazee wa kanisa na jamaa ya Rapong,o kiasi cha kuwasilishwa kotini ambapo koti iliamuru kuwa ,marehemu azikwe akiwa ameketi chini.

1 comment:

ECN RADIO 99.9 FM said...

Waa!! maajabu ya Bungoma kweli