Monday, 24 October 2016

KILONZO:NINA FURAHA KWA KUREJEA UWANJANI TENA.

Oliver Kilonzo.

Na Brian Nyaberi.

Mlinzi wa klabu ya Wazito Oliver Kilonzo ameeleza furaha yake kwa kufaulu kurejea uwanjani baada ya kuwa nje kwa kpindi cha miezi mitano kutokana na jeraha.
Beki huyo alicheza katika kipindi cha pili kwenye mchuano wao na Nakuru All-stars mnamo siku ya Jumapili iliyoisha kwa sare ya bao 1-1 huku akieleza Imani yake kwamba wameimarika kama timu baada yao kutoshindwa katika mechi zao nne zilizopita.

Kurejea kwake kutaipiga jeki safu ya ulinzi ya klabu hiyo ambayo hadi sasa haijafungwa mara moja pekee katika mechi zao kumi za ligi ya daraja la kwanza ya NSL zilizopita.

No comments: