![]() |
Wachezaji wa Kenya wakiwa kwenye mazoezi. |
Na Mwangi Robert.
Kocha
wa Harambee Stars Stanley Okumbi amekitaja kikosi cha wachezaji 25
wanaokipiga kwenye ligi ya nyumbani ili kujiandaa kwa mechi za kirafiki ambazo
timu hiyo imeratibiwa kushiriki.
Vijana
wa Kenya wameratibiwa kuwa wenyeji kwa timu ya Mozambique na Liberia mnamo
tarehe 12 na 15 mtawalia mwezi ujao wa Novemba.
Kando
na mastaa wanaocheza katika ligi kuu ya Kenya Okumbi aidha amewaorodhesha
wachezaji wanaokipiga kwenye ligi ya daraja la kwanza akiwemo mlinzi wa Vihiga
United Bernard Ochieng’ na mwenzake Michael Misigo, kiungo wa Nzoia Sugar
Lawrence Juma na Morven Otinya wa Palos
FC.
Stars wanajiandaa
kwa Dimba la CECAFA Senior Challenge CUP litakaloandaliwa nchini Kenya.
No comments:
Post a Comment