![]() |
Mchezaji wa Chelsea Kurt Zouma. |
Na VIVIAN ATIENO
Baada
ya mchezaji wa Chelsea Kurt Zouma kuwa mkekani kwa kipindi cha miezi minane
sasa mchezaji huyo ameponya jeraha lake huku akiorodheshwa kwenye kikosi chao
cha chipukizi kilichocheza hapo jana.
Zouma
alikuwa amepata jeraha la goti katika sare ya bao 1-1 ya ligi kuu nchini
uingereza dhidi ya Manchester United.
Kimekuwa
kipindi kigumu kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 ambaye amelazimika
kuwatazama wenzake wakicheza huku jeraha hilo likimnyima nafasi ya
kuliwakilisha taifa lake kwenye michuano ya yuro iliyochezwa nyumbani kwao
Ufaransa.
Lakini
Zouma alikuwa amefaulu kurejea mazoezini kabla ya msimu huu kung’oa nanga na
kupata nafasi ya kufanya mazoezi chini ya meneja wake mpya Antonio Conte.
No comments:
Post a Comment