Tuesday, 27 September 2016

HATUBADILI MSIMAMO KUHUSU USIMAMIZI WA CHUO CHA MOI-MANDAG'O

Gavana wa Uasin Gishu Jackson Mandag'o
Ben Kirui

Gavana wa kaunti ya Uasin Gishu Jackson Mandago ameapa kushikilia msimamo wake kuhusu usimamizi wa chuo kikuu cha Moi licha ya kufika katika makao makuu ya CID kuhojiwa.

Haya yanajiri siku moja tu baada ya waziri wa Usalama Joseph Nkaissery kutoa onyo dhidi ya magavana wawili na wabunge kutoka eneo la North Rift.

Hata hivyo baada ya masaa matatu ya mahojiano na maafisa wa ujasusi viongozi hao walisisitiza kuwa lazima uteuzi wa usimamizi wa shule ufanywe kwa njia ya haki huku gavana Mandago alielekezea kidole cha lawama vyombo vya habari kwa kueneza habari zisizo za ukweli.


Wakati huo huo wenyeji kutoka eneo la Eldoret waliandamana kupinga kuhojiwa kwa gavana Mandag’o.

No comments: