Thursday, 27 October 2016

SERIKALI YAJIANDAA KUZIMA WIZI WA MITIHANI YA KITAIFA

Maafisa wa elimu wakiongozwa na mawaziri Matiang'i, Nkaisary na Mucheru.
Robert mwangi.

Waziri wa elimu humu nchini Fred Matiang’i ametoa onyo kali kwa mtu yeyote aliye na mpango wa kuhitilafiana na mitihani ya KCPE na KCSE itakayo fanyika kuanzia mwezi mwezi ujao.

Matiang’i  vilevile amewaonya wakenya walio na mpango wa  kusaidi wanafunzi katika wizi wa mitihani hiyo akisema kuwa watakabiliwa vikali kisheria.

Waziri huyo  akiwa pamoja na waziri wa usalama wa ndani Joseph Nkaisery, na mwenzake wa habari, teknolojia ya mawasiliano Joe Mucheru, wameafikiana  kuwa usalama wa karatasi za mitihani mwaka huu utakuwa wa hali ya juu.

Mtihani wa KCPE utaanza Jumanne  tarehe mosi mwezi Novemba huku mtihani wa  KCSE ukitarajiwa kuanza jumatatu ya wiki itakayo fuata.

No comments: