Wednesday, 16 December 2015

Maiti yalipuka na kuwaka moto!!!

Na KakaMusa,

Wenyeji wa kijiji cha Enyapora Mumias, Kakamega county wamepigwa na butwaa baada ya jeneza kulipuka na maiti kuwaka moto.
Jeneza la Mfu
Kitendo hiki cha kushangaza kilitokea wikendi iliyopita ambapo walikuwa wanajitayarisha kuzika maiti hiyo.


Maiti hiyo ni ya mwanamke wa umri wa makamo ambako walioshuhudia kisa hicho walisema kuwa maiti ilichomeka miguu na pia sehemu ya ndani ya jeneza.

Inadaiwa kuwa mwanamke huyo alikuwa hajafurahishwa na mumewe baada ya mume  huyo kutomjengea nyumba licha ya kumzalia watoto.

Kulingana na mwenyeji wa humo, mwanaume katika jamii ya waluhya ni sharti amjengee nyumba nzuri mkewe ili kumridhisha lakini bwana wa mke huyu hakuwa ametekeleza hilo.

No comments: