![]() |
Athari ya mafuriko, Lunga Lunga, Kaunti ya Kwale, kama ambavyo ilisababishwa na mvua kubwa ya El Nino. |
Watu wengi wamefariki, mali ya dhamana yameharibika, na boma
nyingi zimesalia mahame kufuatia fujo
ya mvua inayoendelea ya Elnino ,ambayo yatabirika kuwa yaweza chukua muda mrefu
kusimama.
Tunapozungumza zaidi ya familia 100 kutoka eneo la Vanga, huko Lunga
lunga, kaunti ya Kwale zimesalia kuwa bila makao, vile vile mazao pamoja na
mifugo yao haikusazwa na wingi na msukumo mkubwa wa maji, kwani ilisombwa Kufuatia mafuriko ya mto wa Maumba.
Kwa maneno yake Mwanaharakati
wa kutetea haki za kibinadamu kutoka Vanga, Mohamed Ferunzi , vitongoji vya
Dziriphe,Kiwegu Chuini ni baadhi ya maeneo yaliothirika zaidi na mafuriko hayo.
Mwanaharakati huyo
aidha ameeleza hofu ya kuangamia kwa mali zaidi iwapo suluhu ya haraka
haitapatikana hususan kuzuia majanga yanayotabiriwa, kwani kwa Sasa taifa la
Tanzania linashuhudia mvua inayotabiriwa kuendelea kwa muda wa miaezi sita
ijayo.
Baadhi ya mambo
yanayonuiwa kuadhiri wakenya iwapo mvua hii itaendelea, ni pamoja na matatizo
ya usafiri, kwani wakati wa mvua washika dau katika sekta ya usafiri hapa
nchini huchukua mwanya huu kuwanyanyasa wasafiri kwa kupandisha nauli kwa
pakubwa, hivyo kufanya kuwa mzigo mkubwa kwa wengi haswa kwa wanaotumia teksi
na pikipiki.
No comments:
Post a Comment