Monday, 11 April 2016

ISAAC RUTO ATAJA HAFLA YA MAOMBI ITAKAYOFANYIKA AFRAHA KAMA YA KUKEJELI WAATHIRIWA

Gavana wa Bomet Isacc Ruto
Ben Kirui

Gavana wa Bomet Isaac Ruto amepinga hafla ya maombi ambayo imepangwa na rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto itakayoandaliwa katika uwanja wa Afraha mjini Nakuru jumamosi ijayo.

Mkutano huo wa maombi ambao Rais Kenyatta alitangaza pindi tu mahakama ya ICC ilipotupilia mbali kesi iliyokuwa ikimkabili Naibu Rais na Mwanahabari Joshua arap Sang’ umetajwa na Gavana Ruto kama wa kukejeli waathiriwa wa ghasia za 2007.


Gavana Ruto badala yake amewataka rais Kenyatta na naibu wake Ruto wawazie kuhusu vile wataunganisha taifa hili na kuliponya kabisa kutokana na athari za muda mrefu za ukabila na misukosuko ya kijamii.

No comments: