Sunday, 7 August 2016

WATANO WAFARIKI, 59 WAKIKWEPA NA MAJERAHA KWENYE AJALI BARABARANI.

Wanawake watano na mvulana mmoja walifariki huku 59 wakijeruhiwa kwenye ajali ya usiku wa kuamkia leo.

Ben Kirui


Watu watano wamefariki huku wengine 59 wakikwepa na majeraha baada ya basi moja kupoteza mwelekeo na kuanguka katika eneo la Ngele Mbooni mashariki kaunti ya Makueni katika barabara kuu ya kutoka Mjini Tawa kuelekea Macii.

Kulingana na OCPD wa Mbooni mashariki James Baraza watatu walifariki papo hapo huku wengine wawili wakifariki wakati wakikimbizwa hospitalini.

Miongoni mwa waliofariki katika ajali hiyo ya usiku wa kuamkia ni wanawake wanne na mvulana mmoja wa miaka 7.

59 waliojeruhiwa wamekimbizwa katika hospitali za Tawaa na wengine katika hospitali ya Makueni level 4.

Baraza amesema huenda basi hilo lilikuwa likiendeshwa kwa kasi.

No comments: