![]() |
Mabaki ya magari yaliyoteketea wakati lori lilipuka |
Ben Kirui
Maafisa 11 wa kitengo cha GSU ni miongoni mwa watu 33
waliofariki Jumamosi usiku kwenye barabara kuu ya Naivasha-Nakuru wakati lori lililokuwa
limebeba bidhaa zinazoshika moto kugonga matuta barabarani na kupoteza
mwelekeo, kisha kugonga magari mengine na kushika moto.
Kwenye taarifa kutoka Ikulu ya Nairobi msemaji wa ikulu Manoa Esipisu amesema kuwa Maafisa hao kutoka kwa kitengo cha Ulinzi wa Rais walikuwa wanasafiri kutoka kaunti ya Bomet ambapo Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto walikuwa wamezuru mapema jana.
Rais Uhuru Kenyatta ametuma ujumbe wa rambirambi kwa familia za wahanga.
No comments:
Post a Comment