![]() |
Mabaki ya matatu iliyohusika katika ajali hiyo ya mapema leo. |
Ben Kirui
Idadi ya watu waliofariki
kufuatia ajali mbaya ya barabarani katika barabara ya Katito-Pap Onditi imeongezeka
na kufikia 14.
Hii
ni baada ya watu watatu zaidi waliokuwa wakipokea matibabu katika hospitali ya Nyabondo
mjini Kisumu kufariki.
Manusura
wengine wanne wanaendelea kupokea matibabu katika kituo hicho ambapo walikimbizwa
baada ya ajali hiyo ya mapema leo asubuhi.
Kwa mujibu wa kamanda wa trafiki mkoani Nyanza, Andres
Naibei, ajali hiyo ilitokea katika eneo la Daima wakati dereva wa matatu kukosa udhibiti na kutumbukia katika mtaro ikiangamiza abiria 11 papo hapo.
Naibei
anasema baadhi ya waathirika walikuwa wanafunzi waliokuwa wakisafiri kurejea shuleni
Matatu
hiyo ilikuwa ikielekea Kisumu kutoka Sirare kaunti ya Migori
No comments:
Post a Comment