Tuesday, 16 May 2017

SHAMBULIZI LINGINE LA KIGAIDI MANDERA.

vijana wanodaiwa kuwa alshabaab
BY RACHEAL KITHAKA

Chifu mmoja  ameripotiwa kuuwawa kufuatia shambulizi linalodaiwa kutekelezwa na magaidi wa kundi Al Shabab katika eneo la Omar Jillo huko Mandera.

Kulingana na kamanda wa polisi wa utawala kaunti hiyo Suleiman Hussein, magaidi hao walivamia nyumba ya chifu huyo saa nne usiku wa kuamkia leo na kumuua kwa kumpiga risasi.

Aidha wahalifu hao wanaarifiwa kuwateka nyara polisi  wawili wa akiba huku ripoti ikiarifu kuwa wamevuka nao na kuelekea katika taifa jirani la Somalia.


wiki moja iliyopita magaidi hawa walimuuwa mchimba migodi katika timbo la Elwak kaunti hiyo, visa hivi vikijiri huku kukiwa na amri ya kutotoka nje ambayo imeongezwa kwa zaidi ya mara mbili na waziri wa usalama Joseph Nkaissery.

No comments: