By Rashid Mwazuma
Mbunge wa Nandi hills Alfred Keter mbunge maalum wa URP Sonia Birdi wanatarajiwa leo katika mahakama ya Naivasha
kushtakiwa kwa kosa la kufanya usumbufu katika kituo cha kupima uzani malori
cha giligili yapata miezi miwili
iliopita.
Hii ni baada ya mahakama kuu kukataa kuwapa
amri waliomba kuzuia kukamatwa na kushtakiwa kwao.
Katika uamuzi wake, jaji Mumbi Ngugi
amesema kwamba wabunge Keter na Birdi wameshindwa kuonyesha jinsi haki zao
zitakiukwa endapo watakamatwa na kushtakiwa na akaagiza washtakiwe kesho .
Kesi hiyo itatajwa tarehe 19 Juni ili
maagizo zaidi yatolewe.

No comments:
Post a Comment