![]() |
| Gavana wa Kisumu Jack Ranguma na wafuasi wa Cord baada ya kutimuliwa na polisi |
Ben Kirui
Wafuasi wa
upinzani wakiongozwa na gavana wa Kisumu Jack Ranguma wamefurushwa na polisi
asubuhi ya leo walipokuwa wakiandamana kuelekea katika afisi za IEBC za kaunti
ya Kisumu kwa nia ya kuwafurusha makamishna wa tume hiyo.
Shughuli za
biashara zilikwama katika mji wa Kisumu wakati wa maandamano hayo huku polisi
wakilazimika kutumia vitoa machozi kuwatawanya wafuasi hao.
Gavana Ranguma
amesema alikuwa anawasilisha nia ya mazungumzo ya kutaka kutolewa kwa maafisa
wa IEBC.
Ranguma ameshtumu
hatua hiyo akisema haitawazuia kuendelea na maandamano ambayo ni halali.

No comments:
Post a Comment