NA ELVIS OWUOR
![]() |
Alshabaab wakipewa amri ya mashambulizi |
Wakenya wametakiwa kuwa waangalifu
msimu huu Krismasi kwa minajili ya usalama wao dhidi ya kundi la wanamgambo wa
alshabaab kujigawanya katika makundi mawili ili kupata ushindi katika maovu
wanayotarajia kutekeleza.
Huku
mbwembwe za kila aina zikionekana kwa wakenya wengi , maeneo ya burudani na masoko
yakiwa yamefurika furi furi sherehe za krismasi
kuanza rasmi Taarifa inayojiri kutoka kwa idara ya usalama nchini inaelezea
jinsi wanamgambo wa Alshabaab wanavyoazimia kutekeleza mashambulizi humu nchini
limepokelewa kwa uangalifu mkuu na inspekta jenerali wa polisi Joseph Boinet.
Boinet
amesema kuwa sasa kundi la alshabaab limejigawanya kwa upande Mbili moja
ikijiunga na wanamgambo wa Islamic State na lingine likiunga mkono Al-Qaeda.
Inadaiwa kundi
la alshabaab linalounga mkono ISIS linafanya operesheni yake Kaunti ya Mandera
huku lile liko nyuma ya Al-Qaeda limekita kambi katika msitu wa Boni ilioko
eneo kusini la Kenya
![]() |
| Boinet adressing press |
Inspekata
Jenerali ameelezea kuwa makundi haya mawili yanashindana kueneza ajenda ya
jihad ambayo itakuwa mbaya zaidi iwapo itatokea.
Vile vile
Boinet amesema kuwa katika basi liliotekwa nyara jumatatu ya wiki hii ambapo
waislamu waliweza kuwakinga wakristo waliokuwa wakisafiri nao eneo la El Wak
kaunti ya Mandera lilfanywa na ISIS.
Aidha
Boinet amesema kuwa genge hilo kutoka mandera linalongozwa na Isaak Osman Ali
almaarufu kama Okola,, Abdifata Basre na Mohamed Bilal huku lile ya Al-Qaeda likiongozwa
na Omar Ahmed Abdumanan.


No comments:
Post a Comment