Sunday, 27 December 2015

WANAMGAMBO WA AL SHAABAB WAZIDISHA UNYAMA, MANDERA. KUNANI?

Na Julius Kariithi

Maafisa wa polisi pamoja na mshirika wa kundi msalaba mwekundu wakibeba mwili wa baadhi ya waliouwawa katika mashambulizi ya  hivimajuzi Mandera.


Tukio lingine la kustajabisha zimejitokeza katika kaunti ya Mandera ambapo maafisa wawili wa usalama wameuwawa na wengine kujeruhiwa kufwatia mashambulizi ya kigaidi yaliyosababishwa na kundi la wanamgambo wa  Al Shabab.
 Gavana wa Mandera ,Ali Ibrahim Roba, alithibitisha mashambulizi hayo yaliyotekelezwa katika eneo la Kurkura, karibu na lungu baina ya mpaka wa, Elwak na Laffe, na kuwauwa maafisa wawili na kuwajeruhi wawili pia.
Ni matukio ya kigaidi ambayo yanazidi kushuhudiwa hapa nchini wakati idara ya polisi inazidi kubambana vikali na maswala ya kigaidi haswa katika msimu huu wa Krismasi.

Mashambulizi haya yanajiri siku moja tu baada ya ya kifo cha gaidi mmoja wa Alshabab, aliyejaribu kutega vilipuzi katika kaunti hiyo ya Mandera.

No comments: