Na KakaMusa
![]() |
| Picha kwa hisani ya The Star. |
Mwanaume amdunga mkewe kwa kutumia kisu kwenye shavu na
kumuumiza mfupa baada ya mzozano wa kifamilia huko Khorof Harar, Kaunti ya Wajir.
Fatuma Ibrahim
yungali na kisu shavuni mwake kwani daktari walidai kuwa hawangeweza kukitoa
kisu hicho kwa ugumu wa kuhatalisha maisha ya mwanamke huyo wa miaka 32.
Ibrahim ambaye ni mama wa watoto wanne atasafirishwa Nairobi
kwa upasuaji katika hospitali kuu ya Kenyatta.
Wanawake walijitokeza kwa wingi kuumpa nguvu Ibrahim na
kuikashifu serikali kwa kudhalilisha haki zao.
“Haki za wanawake ni sharti zizingatiwe ili kuzuia mashambulizi
na dhuruma za kijinsia,” alisikikia akisema mwanamke Sahara Keynan.
Hata hivyo, OCPD
wa Wajir, Benson Mukumbi alisema
kuwa Mohamed Deeq ambaye ndiye
kutekeleza unyama huo tayari ametiwa mbaroni na atafikishwa mahakamani siku ya
ijumaa. #ASANTE

No comments:
Post a Comment