![]() |
| Kiongozi wa upinzani Raila Odinga |
Ben Kirui
KIONGOZI wa CORD Raila Odinga ameisuta serikali kwa kuamuru mamlaka ya ukusanyaji ushuru KPA kufunga vituo viwili vya kuhifadhi shehena vinavyomilikiwa na familia ya gavana wa mombasa Ali Hassan Joho.
Kwenye taarifa aliyotuma kwa vyombo
vya habari Odinga amesema hatua hiyo ni mpango wa serikali ya Jubilee kutisha
na kuhangaisha magavana wa upinzani.
Baadhi ya wabunge wa mrengo wa Cord
wakiongozwa na mbunge wa Mvita Abdulswamad Shariff Nassir nao wamelalamikia
hatua hiyo wakisema imechochewa na mahasimu wa Joho.Kwenye waraka mkurugenzi mkuu wa KPA Gichiri Ndua anasema shughuli katika vituo hivyo imesistishwa kwa muda usiojulikana.
Vituo hivyo ni miongoni mwa vingine vinavyochunguzwa kwani vimehusishwa na wafanyibiashara walaghai wanaoingiza nchini bidhaa za magendo na hata kukwepa kulipa ushuru.

No comments:
Post a Comment