Monday, 21 March 2016

CHIFU WASHAMBULIWA NAKURU.

Pombe haramu.

Chifu mmoja anauguza majeraha katika hospitali ya Nakuru level 5 baada ya kudungwa mkuki mguuni wakati alikuwa  akiendesha kampeni dhidi ya pombe haramu huko Lower Solai kaunti ya Nakuru.


Samuel Totona wa kata ya maji tamu akiandamana na machifu wenzake walishambuliwa na kundi la vijana baada ya kumkamata mshukiwa wa biashara ya pombe haramu katika eneo la Arusto.  


Chifu huyu amelaumu maafisa wa utawala eneo hilo kwa kutohakikisha kuwa washukiwa wanashtakiwa na kumaliza biashara ya pombe haramu.

No comments: