Monday, 21 March 2016

WALIMU WANAOWAADHIBU WANAFUNZI WATACHUKULIWA HATUA.

By Lena Juliet.
Walimu watakaopatikana wakiwaadhibu wanafunzi kinyume na sheria watachukuliwa hatua.
Wizara ya elimu kupitia mkurugenzi wa masuala ya ubora wa elimu Pius Mutisya anasema wanaendelea kupokea ripoti kuhusu kuadhibiwa kwa wanafunzi licha ya adhabu hiyo kupigwa marufuku.
 Anasema wizara ya elimu haitasita kuwachukuliwa hatua za kinidhamu walimu wanaowaadhibu watoto kwa kutumia kiboko na kuwa huenda wakaachishwa kazi.

Anasema walimu hao hawatatetetewa na serikali iwapo watafikishwa kotini. Amewataka walimu kubuni njia nyingine za kuwaadhibu wanafunzi.

No comments: