Tuesday, 22 March 2016

Bentaleb kuwa nje kutokana na jeraha la goti.



Mwangi K. Githinji.
Kiungo wa Tottenham Nabil Bentaleb atakuwa nje kwa kipindi cha wiki sita baada ya kufanyiwa upasuaji katika goti lake.
Mchezaji wa Tottenham Nabil Bentaleb.
Kiungo huyo alipata jeraha hilo alipokuwa anachezea timu yao ya vijana chini ya umri wa miaka 21 waliyshindwa mabao 3-0  na Leicester japo anatarajiwa kurejea kwenye mazoezi kabla ya msimu huu kumalizika.

Bentaleb ambaye ni mchezaji wa kimataifa wa Algeria amechezea Tottenham mechi mbili pekee msimu huu baada ya kupata jeraha katika majira ya moto lililomuweka nje kwa miezi mitatu.
Kwingineko ni kuwa nyota wa timu ya Arsenal Mesut Ozil amepuzilia mbali madai kwamba anapanga kuondoka klabuni hicho ikiwa Arsene Wenger ataendelea kuwafunza miamba hao wa uingereza.

Kiungo huyo mjerumani ayesajiliwa na Wenger kutoka Real Madrid kwa ada ya yuro milioni 42.5 mnamo mwaka wa 2013  ameeleza kuwa bado anamheshimu sana kocha huyo.

Tayari Ozil ameshinda mataji mawili ya  FA tangu alipojiunga na Arsenal na anakaribia kuvunja rekodi iliyowekwa na Thierry Henry ligini uingereza ya kusaidia kufungwa kwa magoli mara mengi zaidi.


  

No comments: