Tuesday, 29 March 2016

MAKUNDI YA KINA MAMA, WALEMAVU NA VIJANA KUNUFAIKA NA PESA ZA BIASHARA MOMBASA.




By Lena J.

Makundi ya kinamama, vijana na walemavu kaunti ya Mombasa yanatazamiwa kufaidi na shilingi bilioni mbili zilizotengwa na serikali kusaidia kuboresha miradi inayoendeshwa na makundi hayo.
Kaunti ya Mombasa imetengewa shilingi milioni arobaini na sita ambazo zimepangwa kugawanywa kwa makundi yote yaliyosajiliwa na ambayo tayari yanaendeleza miradi mbali mbali.
Haya yamesemwa na  mwenyekiti wa makundi ya walemavu eneo bunge la changamwe James Karanja,  amabaye amesema makundi yatakayo pokea fedha hizo hayahitaji kuzilipa tena kwa serikali, hivyo kuyahimiza makundi ya walemavu kutoogopa na kujitokeza kwa wingi ili wafaidi na mpango huo.

No comments: