![]() |
| kituo cha polisi |
By Lena J.
Vituo tisa vya polisi vitajengwa
katika maeneo tofauti kaunti ya Lamu ili kuimarisha usalama na kurejesha
utulivu kutokana na mashambulizi ya kila mara kutoka kwa waasi wa alshabaab.
Haya ni kwa mujibu wa James Ole
Serian anayeongoza oparesheni dhidi ya waasi hao katika msitu wa Boni.
Ole Serian anasema vituo hivyo
vitafunguliwa katika maeneo ya Bothei Pandanguo na Mananguo. Anasema wanazuilia
washukiwa kadhaa walionaswa katika maeneo ya Lamu, Garsen, Boni na Baragoni
kufuatia oparesheni hiyo.
Ole Serian anasema ili kuleta
utulivu serikali imetuma naibu kamishna wa kaunti hiyo pamoja na wasaidizi 12
katika maeneo ya Ijara, Hulugho, Lamu mashariki na Lamu.

No comments:
Post a Comment