Friday, 4 March 2016

KAMPENI ZA MKONDO WA LALA SALAMA MALINDI.



Vinara wa Cord wakimpigia debe Willy Mtengo

 BEN KIRUI

Joto la kisisasa linazidi kupanda huku zikisalia siku za kuhesabu kabla ya wenyeji wa kaunti za Malindi na Kericho kuelekea kwenye debe kuamua mbivu na mbichi kwenye kinyang’anyiro cha useneta.
Muungano wa CORD umepiga kambi Malindi kumpigia debe Willy Mtengo atakayepeperusha bendera ya chama cha ODM.
Vinara wa CORD Raila Odinga na Kalonzo Musyoka waliongoza kampeni hizo katika eneo la Mwachiche kaunti ya Malindi ambapo waliwarai wenyeji kumchagua Willy Mtengo.
Wakaazi wa Kaunti za Malindi na Kericho wataenda debeni siku ya jumatatu kwa uchaguzi mdogo wa useneta kuziba pengo zilizoacha wazi na Dan Kazungu Kambi na Charles Keter mtawalia ambao waliteuliwa kuwa mawaziri.
Huku hayo yakiarifiwa mgombeaji wa chama cha Jubilee katika uchaguzi mdogo wa Malindi Philip Charo, amepigwa jeki baada ya wagombeaji wawili kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho ili kumuunga mkono.
Wagombeaji hao, Peter Ponda wa Chama Cha Uzalendo na Fuad Kombe wa Federal Party of Kenya, wamesema wameamua kujiondoa ili kumuunga mkono mgombeaji huyo wa Jubilee.

1 comment:

Anonymous said...

Itakuwa vigumu sana kwa Charo ikizingatiwa kwamba Malindi ndio ngome ya Cord