Monday, 7 March 2016

POLISI WACHUNGUZA KUHONGA KWA WAPIGA KURA MALINDI.


Mbunge wa Lamu Mashariki Shariff Athman.

By Lena Juliet
  
Maafisa wa polisi huko malindi wanachunguza madai mbali mbali ya kuwapa wapiga kura hongo katika uchaguzi mdogo unaoendelea mjini humo.
Polisi walilazimika kufyatua risasi hewani katika tukio moja ili kutawanya kundi la vijana lililomshambulia mbunge wa Lamu Mashariki Shariff Athman baada ya madai ya kununua wapiga kura.
Mbunge wa Mwea Peter Gitau pia ameokolewa kutoka mikononi mwa raia hususan wafuasi wa ODM ambao walimtumuhumu kwa kuwapa wapiga kura hongo kabla hajawasilisha malalamishi katika kituo cha polisi cha Kilifi.


No comments: