![]() |
| Benki ya Chase ilifungwa na kuwekwa chini ya urasimu |
Ben Kirui
Afueni kwa wateja wa benki ya chase
baada ya benki kuu ya Kenya kutangaza kwamba wateja hao wataweza kupokea huduma
za benki hiyo siku ya jumatano wiki ijayo.
Benki hiyo iliyowekwa
chini ya urasimu majuma mawili yaliyopita itafunguliwa kufuatia makubaliano
baina ya benki ya KCB na washika dau wengine kuchukua hisa za benki zake.
Gavana wa benki kuu ya Kenya Dkt Patrick Njoroge ametangaza kuwa matawi
yote 62 ya benki hiyo, yatafunguliwa tena ifikapo tarehe 27 mwezi huu.
Hata hivyo wateja
wataruhusiwa kutoa hadi shilingi milioni moja huku wanaotaka kutoa zaidi ya
milioni moja watasubiri hadi mchakato wa kuweka mkakati wa kupata fedha hizo
utakapokamilika.

No comments:
Post a Comment