![]() |
| Washukiwa hao wamekuwa miongoni mwa genge ambalo limekuwa likihangaisha wakaazi |
Ben Kirui
Washukiwa wanane wa ujambazi wameuawa
kwa kupigwa risasi na maafisa wa polisi katika mtaa wa Mukuru kwa Reuben.
Katika kisa
hicho cha usiku wa kuamkia leo, bunduki nne, visu viwili, simu 12 za rununu ambazo
zinaaminika kuibwa pamoja na sare rasmi ya polisi zilinaswa kutoka kwa majambazi
hao.
Kulingana na
kamanda wa polisi wa eneo la viwandani Nehemiah Langat, washukiwa hao ni
miongoni mwa genge ambalo limekuwa likihangaisha wakaazi kwa muda.

No comments:
Post a Comment