Tuesday, 19 April 2016

AGA KHAN KUWATIBU WAGONJWA WA SARATANI KUTOKA UGANDA

Mashine ya kutibu saratani katika hospitali ya Aga Khan
Ben Kirui

Hospitali ya Aga Khan imeahidi kuwalipia matibabu wagonjwa wa saratani kutoka nchini Uganda kufuatia kuharibika kwa mashine inayotibu ugonjwa huo nchini Uganda.

Hospitali hiyo imesema kwamba inaweza toa huduma ya matibabu kwa idadi ndogo ya wale wanaohitaji uuguzi.


Serikali ya Uganda tayari ilikuwa imetangaza kuwa itawasafirisha wagonjwa hao kupata matibabu humu nchini.

No comments: