Tuesday, 19 April 2016

MAHAKAMA YA ICC YATISHIA KUCHUKULIA KENYA HATUA KALI

Mahakama ya Kimataifa ua Uhalifu (ICC)
Ben Kirui

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imetishia kuchukulia Kenya hatua kali iwapo haitasalimisha kwa mahakama hiyo washukiwa watatu wanaokabiliwa na mashtaka ya kutatiza mashahidi.

Msemaji wa ICC Fadi el Abdalla amesema mahakama hiyo itaripoti Kenya kwa baraza la mataifa wanachama wa mkataba wa Roma iwapo serikali itashikilia msimamo wa rais Uhuru Kenyatta wa kutowasilisha wakenya hao watatu mbele ya mahakama hiyo.

Kiongozi wa mashataka wa ICC Fatou Bensouda tayari amepata kibali cha kuwakamata aliyekuwa mwanahabari Walter Baraza, wakili Paul Gicheru na Philiph Bett kwa madai ya kutatiza mashahidi katika kesi dhidi ya naibu Rais William Ruto na mwanahabari Joshua Sang’.


Akihutubia hafla ya maombi ya shukrani iliyofanyika katika uwanja wa Afraha mjini Nakuru siku ya jumamosi baada ya kutamatishwa kwa kesi za wakenya kule ICC, rais Kenyatta alisema kuwa hakuna mkenya yeyote ambaye atafikisha katika mahakama ya ICC kujibu mashtaka.

No comments: