Thursday, 14 April 2016

WACHA KUCHAFULIA TAIFA JINA RAIS AMUONYA RAILA.

Rais Uhuru Kenyatta
Ben Kirui

Rais Uhuru Kenyatta amemtaka kinara wa Cord Raila Odinga kuacha kuchafulia taifa hili jina wakati wowote anapozuru nchi za ngambo.
Hii ni kufuatia matamshi ya Raila kwamba ICC ilikosea kwa kufutilia mbali kesi iliyokuwa ikikabili wakenya sita katika mahakama ya ICC katika mahojiano na kituo kimoja cha televisheni nchini Ufaransa.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika kaunti ya Nyandarua, Rais alionekana kukerwa na matamshi ya Raila akisema ikiwa mahakama ya ICC iliridhika kuwa naibu rais William Ruto na Joshua Sang’ hawakuwa na kesi ya kujibu sio sawa kwa Raila kuendelea kuikosoa mahakama hiyo kwa uamuzi wake.


Kwa upande mwingine naibu wake William Ruto alisema hatua ya ICC kutupilia mbali kesi iliyokuwa ikimkabili imewakera mahasimu wao kisiasa ambao walidhania wangepata fursa ya kuiongoza taifa hili ikiwa mambo yangeenda mrama

No comments: