Wednesday, 13 April 2016

WANAFUNZI 139 ZAIDI WA CHUO CHA NAIROBI WAFURUSHWA.

Wanafunzi zaidi wa chuo kikuu cha Nairobi wafurushwa kwa kuhusishwa na ghasia zilizozuka chuoni.
Chuo kikuu cha Nairobi kimewarejesha nyumbani wanafunzi 139 zaidi siku moja baada ya wanafunzi 62 kupewa ilani ya kutimuliwa.
Chuo hicho kimetaja hatua hiyo kama ya kinidhamu dhidi yao kwa kuhusika katika ghasia na uharibifu wa mali, kufuatia ghasia na fujo zilizoshuhudiwa katika bewa lake kuu baada ya uchaguzi wa mwenyekiti wa chama cha wanafunzi SONU.

Wanafunzi ambao wamehusishwa wameagizwa kuchukuwa barua za kufurushwa kwao kutoka bewa kuu la chuo hicho kufikia ijumaa wiki hii.

No comments: