Monday, 30 May 2016

Nkaissery atoa onyo kwa viongozi wa CORD.







Na Editer Wakesho


Waziri wa maswala ya usalama wa ndani Joseph Nkaissery amesema polisi watawatia  pingu vinara wa CORD, endapo watakwenda kinyume cha sheria.


Nkaissery amesema serikali imeipa CORD muda  mwingi wa kujieleza kwa mapendekezo yao, walakini sasa haitaruhusu yeyote kujihusisha na ukiukaji wowote wa kisheria na vitisho vinavyoelekezwa kwa serikali.
Aidha Nkaissery amesema Raila Odinga, Moses Wetangula, Kalonzo Musyoka na seneta wa Siaya James Orengo na mwenzake wa Machakos Johstone Muthama watashikwa endapo watavunja sheria akiongezea kuwa hawataruhusiwa kuandaa mkutano wowote katika bustani ya Uhuru.

Pia alisema  kuwa ni rais pekee aliye na mamlaka ya kuongoza sherehe sampuli ya Madaraka wala sio yeyote mwingine..

Matamshi yake Nkaissery yanakuja huku mvutano ungali ukiendelea kutokota kuhusu ni nani atakayeruhusiwa kuandaa mkutano katika bustani ya Uhuru kati ya CORD na kanisa la Prayers Beyond Boundaries linalodai kwamba lilikuwa la kwanza kutwaa ruhusa ya kuitumia. 


No comments: