Monday, 13 June 2016

BAADA YA ZLATAN MOU SASA ANAMTAKA VERRATTI.


Nyota wa PSG Marco Verratti.



Mwangi K.Githinji.

Manchester United wameanza kumtupia jicho kiungo wa Paris Saint-Germain Marco Verratti .

Inakisiwa kuwa United wanatayarisha dau la pauni yuro milioni 79 ili waweze kumshawishi ajiunge nao.
Verratti mwenye umri wa miaka 23 ameichezea PSG mara 157 tangia alipocheza mechi yake ya kwanza mnamo mwaka wa 2012 akiwa bado chipukizi.
Inaaminika kuwa kocha Jose Mourinho ni shabiki mkubwa wa Muitalia huyo ambapo yupo makini kuona kuwa anakipiga na klabu chake msimu ujao.


Iwapo watamtwaa  Verratti, watamlipa donge nono la yuro milioni 6.7 kwa msimu huku ikielezewa kuwa mchezaji Zlatan Ibrahimovic anataka wahamie united pamoja.

No comments: