![]() |
| Mchezaji wa Manchester United Michael Carrick. |
Mwangi K .Githinji.
Kiungo wa Manchester United Michael Carrick amesaini
mkataba wa mwaka mmoja na klabu hicho.
Kiungo
huyo mwenye umri wa miaka 34 alipewa nyongeza ya mkataba huo na kocha mpya Jose
Mourinho ambaye anaamini kuwa bado Carrick atakuwa nguzo muhimu
anapojitayarisha kwa msimu mpya.Carrick
alijiunga na United kutoka Tottenham mnamo mwaka wa 2006 na amefaulu kushinda
mataji matano ya ligi na lile na klabu bingwa barani ulaya.Baada
ya kusaini nyongeza hiyo kiungo huyo alieleza furaha yake kwa kupata nafasi ya
kuichezea united huku akimtaja Jose kama kocha aliye na umahiri wa kushinda
mataji kila aendapo.

No comments:
Post a Comment