![]() |
| Mchezaji Alvaro Morata. |
Mwangi K. Githinji.
Chelsea
wanawinda sahihi ya mchezaji wa Juventus Alvaro Morata wakati dirisha la uhamisho
litakapofunguliwa.
Morata amefunga mabao 27
katika mechi 93 alizochezea Juve tangia alipojiunga na miamba hao wa ligi kuu
ya nchini Italia mnamo mwaka wa 2014 ,lakini kwa muda sasa ameendelea kuhusishwa
na uhamisho wa kuvighuria vilabu kadhaa vinavyoshiriki ligi ya uingereza.
Inakisiwa kuwa donge
nono la mshahara na pia ujio wa meneja mpya Antonio Conte huenda ukamshawishi
kuenda Chelsea
Aidha mwakilishi wake
alisafiri ugani Bernabeu ijumaa iliyopita ili kufanya mazungumzo na klabu cha
Real Madrid.

No comments:
Post a Comment