Friday, 17 June 2016

AZIMIO LANGU SI KUHAMIA ARSENAL MBALI UNITED-MKHITARYAN.



Nyota wa Dortmund  mkhitaryan

Mwangi K.Githinji. 

Vilabu vya Manchester United na Arsenal vimeingia katika vita mgao wa kula baada ya ajenti wake kufichua kwamba staa wa Dortmund Henrikh Mkhitaryan angependelea kuhamia United.

Miamba hao wa ujerumani walidhibitisha usiku wa jana kuwa mchezaji huyo amekataa kusaini mkataba mpya na klabu hicho huku kandarasi yake ikitarajiwa kukamilika mwishoni mwa msimu wa 2017.

Itawalazimu Dortmund kufanya uamuzi wa kumuuza ama kuendelea kumbakiza nyota huyo ama wampoteze baada ya kipindi cha miezi 12, bila kulipwa ada yoyote.

Habari hizo ni pigo kwa Arsenal ambao wanasaka sahihi ya nyota huyo Mkhitaryan aliyekuwa anachezea klabu cha Shakhtar Donetsk hapo awali.


No comments: